Nenda kwenye maudhui
RAFIKI WA FAMASIA YAKO

Famasia yako. Dawa, pesa na timu, sehemu moja.

Mauzo, stoo, expiry za dawa, supplier, zamu na ripoti, vyote sehemu moja. Unajua kinachoendelea dukani kwako bila kubahatisha.

Kila mtu anaona kazi yake.
Mmiliki, mfamasia na timu, kila mmoja na ruhusa yake, rekodi moja.

Lucresia Pharmacy · KariakooMO
JUMATANO, 29 AGOSTIHabari, Michael
MAUZO LEOTSh 842,500↗ 12.4%
FAIDA MAKADIRIOTSh 218,40026% margin
WATEJA474 wanasubiri
Mauzo ya siku 7TSh 4.8m
AlJtJnAlhIjJmJp
Angalia hivi leo3
  • 14Expiry inakaribiaNdani ya siku 60
  • 6Stoo imepunguaChini ya kiwango
  • 2Zinasubiri idhiniAngalia sasa
STOO SALAMAHakuna dawa iliyokwisha leo
MAUZO YAMEKAMILIKATSh 18,500

Kiswahili kwanzaRahisi kufundisha timu

Inafanya kazi kwenye simuSimu, tablet na kompyuta

Kila hatua ina mwenyeweRekodi kamili za kazi

Backup na updatesVipo ndani ya kifurushi

SI MFUMO WA MAUZO TU

Famasia nzima inaongea lugha moja.

Ukiuza dawa, Rafiki inasasisha stoo, pesa, historia ya mteja na ripoti ya mmiliki, yote kwa mara moja. Hakuna kuandika kitu kilekile sehemu tatu.

02

Kaunta ya haraka, salama

Tafuta dawa haraka, kagua usalama wa mteja, pokea malipo, toa risiti, foleni inaendelea kusonga.

03

Mmiliki anaona biashara

Mauzo, faida, matumizi, madeni ya supplier na hatari, vyote vimekusanywa tayari kwa maamuzi yako.

04
MOMFMH

Kila kazi, ruhusa yake

Mmiliki, mfamasia, mhasibu na mhifadhi wa stoo hawaingiliani, lakini rekodi zinaungana.

05

Nunua kutokana na uhitaji halisi

Panga manunuzi kutokana na mauzo, stoo iliyopungua na dawa walizoulizia wateja ukawa huna.

06

Ushahidi, si kumbukumbu tu

Kila idhini na kila badiliko limeandikwa: nani, lini, tawi gani, kifaa gani.

MFUMO MMOJA. KAZI TOFAUTI.

Mmiliki anaongoza biashara. Mfamasia anaongoza dawa.

Rafiki haimpi kila mtu kila kitu. Inampa kila mtu anachohitaji kufanya kazi yake vizuri, na inalinda mambo yasiyo yake.

MO
MmilikiRipoti, bei, supplier, malipo, wafanyakazi
MF
MfamasiaKaunta, dawa, wateja, stoo, zamu
MH
Mhasibu na timuWanaona kazi zao tu, sio siri za biashara
rafiki.Lucresia PharmacyMO
MWONEKANO WA MMILIKI

Biashara yako leo

MauzoTSh 842,500↗ 12.4%
Pesa dukaniTSh 626,000Zamu 2 wazi
TawiMauzoHali
KariakooTSh 842,500Vizuri
MbeziTSh 614,000Vizuri
ANZA BILA KUPOTEA

Kutoka usajili hadi mauzo ya kwanza.

Rafiki inakuongoza hatua kwa hatua. Hauhitaji kuwa mtaalamu wa kompyuta.

  1. 01

    Fungua akaunti

    Weka jina lako, namba ya simu na password.

  2. 02

    Lipia kifurushi

    TZS 35,000 kwa mwezi, au lipia miezi 6 na mwaka kwa punguzo. Unalipa salama kwa simu au kadi.

  3. 03

    Weka taarifa za duka

    Weka tawi, leseni, mmiliki na mfamasia wako aliyesajiliwa.

  4. 04

    Weka dawa, anza

    Ingiza dawa kwa CSV au moja moja, kisha anza kuuza.

BEI WAZI

Kifurushi kimoja. Famasia nzima.

Hakuna kulipia kila kitu kivyake. Unapata kila unachohitaji kuendesha tawi lako na timu yako.

i

Kabla ya kuanzaAndaa leseni ya famasia, taarifa za mfamasia aliyesajiliwa, bei zako na stoo ya kuanzia.

TZS35,000/ mwezi
  • Mwezi 1TZS 35,000
  • Miezi 6TZS 140,000unaokoa TZS 70,000
  • Mwaka 1TZS 300,000unaokoa TZS 120,000

Kwa famasia inayotaka control bila usumbufu.

  • Tawi 1 la famasia
  • Hadi wafanyakazi 10
  • Hadi vifaa 5
  • Mauzo, stoo, expiry na dawa
  • Supplier, matumizi na ripoti
  • Backup, updates na msaada
  • Siku 7 za neema baada ya kuisha
Anza na Rafiki Malipo yakithibitishwa tu, famasia yako inafunguka.
WAZI TANGU MWANZO

Rafiki inakusaidia kuamua. Haichukui nafasi ya mtaalamu.

  • 01

    Mfamasia bado anaamuaKupanga madaraja ya dawa, dawa za cheti na maamuzi ya kitaalamu, hayo yanahitaji mfamasia aliyesajiliwa.

  • 02

    Taarifa sahihi ni muhimuRipoti zinakuwa sahihi kama mauzo, stoo, bei na matumizi vimeingizwa sawasawa.

  • 03

    TRA ni mfumo tofautiRafiki haitoi risiti ya TRA mpaka kuwe na muunganisho rasmi uliothibitishwa.

FAQ

Maswali kabla ya kuanza.

Hujapata jibu? Tuandikie support@rafiki.co.tz

Je, Rafiki ni mfumo wa mauzo tu?+

Hapana. Mauzo ni sehemu moja tu. Rafiki pia inaendesha stoo, expiry, dawa, supplier, manunuzi, zamu, matumizi, ruhusa na ripoti za mmiliki.

Mmiliki na mfamasia wanaona kitu kilekile?+

Hapana. Mmiliki anaona upande wa biashara. Mfamasia anaona kaunta, dawa, wateja, stoo na zamu. Kila mtu na kazi yake, kila mtu anawajibika.

Naweza kutumia simu yangu?+

Ndiyo. Rafiki inafanya kazi kwenye simu, tablet na kompyuta kupitia browser, hakuna programu ya kupakua.

Kifurushi kikiisha inakuwaje?+

Unapata siku 7 za neema kulipia upya. Zikipita, akaunti inasimama mpaka malipo yathibitishwe. Rekodi zako hazifutwi.

Naweza kuingiza stoo kutoka Excel?+

Ndiyo. Save faili yako kama CSV, ipakie, kagua kila mstari, kisha uthibitishe ndipo dawa na stoo ziandikwe.

Famasia yako inastahili Rafiki.

Anza leo, ujue dawa zako ziko wapi, pesa iko wapi na timu inafanya nini.

Fungua akaunti